Tuesday, September 18, 2018

SEMINA YA MAPITIO NA UTUNGAJI WA SERA MPYA YA MASHIRIKA YASIYOKUWA YA KISERIKALI

Shirika la Door of Hope to Women and Youth Tanzania ni miongoni mwa Mashirika yaliyopata fursa ya kushiriki kwenye mchakato wa kupitia na kutoa maoni ya uboreshaji wa sera ya Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali na kupata nafasi ya kuudhuria kikao kazi cha siku mbili Bungeni Dodoma ili kupitia kwa kwa kina pamoja na wadau wengine maeneo ya msingi ya uzingatiaji kwenye utungaji wa sera mpya. Tayari kikao kazi kimemaliza uandaaji wa Rasimu ya Sera tayari kwa kuiwasirisha kwenye Wizara husika kama pendekezo la wadau wa sekta. Kikao hiki kimeudhuriwa na Shirika mbalimbali kutoka Tanzania bara, Maafisa wa serikali, Msajiri wa NGOs na kimendaliwa na Baraza la Taifa la mashirika yasiyokuwa ya kiserikali (NaCoNGO).
Image may contain: 4 people, people smiling, people sitting and indoor
Pembeni Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika  la DOOR OF HOPE akifuatilia mjadala kwenye Ukumbi wa BUNGE - DODOMA
Image may contain: 2 people, people sitting

No comments:

Post a Comment

MKURUGENZI WA DOOR OF HOPE AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MHE. WAZIRI MKUU WA TANZANIA

Katika jitihada za kushirikisha wadau na viongozi wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Watanzania kazi na programu zinazotekelezwa na Shir...